Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Bw. Crispin Francis Chalamila anahudhuria mkutano wa kuzindua ‘Jukwaa la Wataalamu wa Urejeshaji Mali Afrika – (Africa Asset Recovery Practitioners’ Forum – AARPF).
Jukwaa hili litatumika kukutanisha wataalamu wanaohusika na ufuatiliaji na urejeshaji mali na kuwawezesha kuwa na sauti moja katika kufuatilia na kurejesha mali zilizopatikana kwa njia haramu ikiwemo rushwa, ndani na nje ya Afrika.
Katika Mkutano huu Mkurugenzi Mkuu ameambatana na Bi. Lilian William Kafiti kutoka Kitengo cha ATRU (DLS) aliyehudhuria kama Rais wa Asset Recovery Inter – Agency Network for Eastern Africa – ARNEA pamoja na Bw. Nathanael Otieno kutoka Kitengo cha ATRU (DLS) ambaye amechaguliwa kuwa ‘Focal Point’ wa Taasisi katika jukwaa hilo.
Mkutano huu ambao umeandaliwa na AU Advisory Board against Corruption – AUABC, unafanyika Nairobi Kenya kuanzia Aprili 15, 2025 na utahitimishwa leo Aprili 17, 2025.