MAAFISA UTUMISHI WAASWA KUDHIBITI RUSHWA YA NGONO MAHALI PA KAZI

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Juma Mkomi amewataka Maafisa wanaosimamia utumishi na rasilimali watu Serikalini, kutekeleza wajibu wao pasipo upendeleo wala kudai rushwa.
Bw. Mkomi ameyasema haya wakati wa ufunguzi wa Warsha ya Kujadili Mkakati wa Kudhibiti Rushwa ya Ngono Mahala pa Kazi iliyofanyika Julai 2, 2024 jijini Dodoma.
Pia amewataka washiriki wa warsha hiyo ambao wengi wao ni Wakurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu kutoka Wizara na Taasisi za Serikali, kutengeneza Mkakati madhubuti wa kudhibiti vitendo vya rushwa ya ngono kwenye maeneo yao unaotekelezeka na wenye kuleta tija kwa Taifa.
Nae Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU CP Salum Hamduni lengo la warsha hiyo ni kuwasilisha matokeo ya utafiti ulifanywa na TAKUKURU pamoja na wada wengine kuhusu rushwa ya ngono katika baadhi ya taasisi nchini ili kupata picha ya namna hali ilivyo na hatimaye kuwawezesha wadau wa warsha hii kuweka mkakati wa namna ya kuzuia na kupambana na vitendo vya rushwa ya ngono katika utumishi wa umma.
Mkurugenzi Mkuu amesema katika eneo la utafiti, TAKUKURU kwa kushirikiana na Taasisi ya Women Fund Tanzania Trust – WFT ilifanya utafiti katika Vyuo Vikuu saba (7), na katika sekta ya elimu kwa walimu wa shule za msingi na sekondari kwa malengo mahsusi ya Kubaini uwapo, sababu, mbinu na wahusika wa vitendo vya rushwa ya ngono.
Pamoja TAKUKURU wadau wengine ambao WSP, TAMWA nao walifanya utafiti katika eneo hili la rushwa ya ngono.

Taarifa kwa Umma