SITA WAHUKUMIWA KWA RUSHWA KONDOA – DODOMA

Septemba 26, 2023, Mahakama ya Wilaya Kondoa, kupitia Hakimu Mwandamizi FEISAL KAHAMBA, amewahukumu washtakiwa sita ambao ni
1.BASHIRU HASSANI DINA aliyekuwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Madege

  1. MUTAPHA ISSA NJORO Mjumbe wa Serikali ya Kijiji
  2. OMARI ABDALLAH MAFITA Mjumbe wa Serikali ya Kijiji
  3. KASIM HASSANI MSENGI – Mjumbe wa Serikali ya Kijiji
  4. MAJID ISSA NJORO – Mjumbe wa Serikali ya Kijiji pamoja na
  5. ABDALA IDD ABDALA
    Mtendaji wa Kijiji cha Madege.

Wamehukumiwa kwa makosa ya matumizi mabaya ya mamlaka kinyume na k/f cha 31 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura ya 329 Marejeo ya 2022 na kukisababisha Kijiji hasara.

Washtakiwa waliuza shamba la Kijiji kwa sh milioni 2 bila ya kufuata utaratibu.

Kila mshtakiwa amehukumiwa kwenda jela miaka 3 au kulipa faini ya sh milioni 2 kila mmoja.

Taarifa kwa Umma