TAKUKURU
No Result
View All Result
  • MWANZO
  • KUHUSU SISI
    • SALAMU ZA MKURUGENZI MKUU
    • HISTORIA YA TAASISI
    • MUUNDO WA TAASISI
    • OFISI ZETU
  • UZUIAJI RUSHWA
  • UELIMISHAJI
  • UCHUNGUZI
  • WASHIRIKA
  • MACHAPISHO
  • Huduma
    • E-Huduma
    • E-Malalamiko
  • BLOGU
Taarifa kwa Umma
  • MWANZO
  • KUHUSU SISI
    • SALAMU ZA MKURUGENZI MKUU
    • HISTORIA YA TAASISI
    • MUUNDO WA TAASISI
    • OFISI ZETU
  • UZUIAJI RUSHWA
  • UELIMISHAJI
  • UCHUNGUZI
  • WASHIRIKA
  • MACHAPISHO
  • Huduma
    • E-Huduma
    • E-Malalamiko
  • BLOGU
No Result
View All Result
TAKUKURU
No Result
View All Result
Home Taarifa kwa Umma

MAAFISA BIASHARA HALMASHAURI YA MANISPAA YA BUKOBA WASHTAKIWA KWA UHUJUMU UCHUMI

MAAFISA BIASHARA HALMASHAURI YA MANISPAA YA BUKOBA WASHTAKIWA KWA UHUJUMU UCHUMI

Maafisa Biashara hao Richard Lubega Kubona, Adelina Kasigwa Leonard na Musa Said Kalumba, wamefunguliwa Kesi ya Uhujumu Uchumi (ECO. Na. 07/2023) Septemba 20, 2023, katika Mahakama ya Hakimu Mkaazi Bukoba Mkoani Kagera, mbele ya Hakimu Mfawidhi Mhe. Janeth Massesa.

Washtakiwa wote wamesomewa makosa ya kutumia madaraka vibaya, ubadhirifu, ufujaji pamoja na matumizi ya nyaraka kumdanganya mwajiri, Kinyume na vifungu vya 22, 28 na 31 vya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Cap 329 R.E 2022), vikisomwa pamoja na vifungu vya Uhujumu Uchumi Aya ya 21 jedwali la kwanza, kifungu cha 57 (1) na 60 (2) Sura ya 200 Marejeo ya Mwaka 2022.

Pia walisomewa shtaka la Utakatishaji Fedha Shs Milioni Mia Nne na Tisa Laki Nne Tisini na Saba Mia Moja Sitini na Tano (sh. 409,497,165/-), mali ya Manispaa ya Bukoba – Kinyume na kifungu cha 12 (1)(d) na 13 (1)(a) vya Sheria ya Kuzuia Utakatishaji Fedha Sura ya 432 Marejeo ya 2022, vikisomwa pamoja na Sheria ya Uhujumu Uchumi Aya ya 22 Jedwali la Kwanza na kifungu cha 57(1) na 60 (2).

Mengine ni Kughushi kinyume na vifungu vya 333, 335 (a) na 337 vya Sheria ya Kanuni za Adhabu Sura ya 16 Mapitio ya 2022.

Kosa lingine ni kuisababishia mamlaka (Manispaa ya Bukoba) hasara, kinyume na Aya ya 10 (1) Jedwali la Kwanza na kifungu cha 57(1) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi sura ya 200 Mapitio ya 2022

Wanashtakiwa kwa makosa hayo kwa kukusanya mapato ya Manispaa ya Bukoba na kufuja kwa manufaa yao, huku wakidanganya kuwa jumla ya Sh 409,497,165/- ziliwekwa katika Benki ya NMB Bukoba akaunti ya Manispaa, huku wakijua kuwa ni uwongo.

Washtakiwa hawakuruhusiwa kujibu chochote kwa sababu mahakama ile haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo, hivyo wamepelekwa rumande hadi Oktoba 4, 2023 litakapotajwa tena.

Shauri hili linaendeshwa na Wakili Kelvin Murusuri akisaidiana na Jacob Daudi kutoka TAKUKURU.

ShareTweetSendShare

Taarifa kwa Umma

MAAFISA BIASHARA HALMASHAURI YA MANISPAA YA BUKOBA WASHTAKIWA KWA UHUJUMU UCHUMI

MAAFISA BIASHARA HALMASHAURI YA MANISPAA YA BUKOBA WASHTAKIWA KWA UHUJUMU UCHUMI

KIKAO KAZI

KIKAO KAZI

SITA WAHUKUMIWA KWA RUSHWA KONDOA – DODOMA

WATATU WAHUKUMIWA KWA RUSHWA KONDOA

KUTOKA MAHAKAMA YA WILAYA MOSHI, KILIMANJARO.

KUTOKA MAHAKAMA YA WILAYA MOSHI, KILIMANJARO.

Habari Motomoto

  • National Governance and Corruption Survey (NGACS) 2020

    National Governance and Corruption Survey (NGACS) 2020

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFUNZO YA AWALI YA UCHUNGUZI YAMEHITIMISHWA RASMI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaotafutwa na TAKUKURU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFUNZO YA “INTERMEDIATE INVESTIGATION COURSE” YAFUNGULIWA RASMI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KIKAO CHA USHIRIKIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

WASILIANA NASI

MKURUGENZI MKUU
TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA
NA RUSHWA
S. L. P 1291
41101 Mtaa wa Jamhuri,
DODOMA, Tanzania
Simu: (026) 2323316
Nukushi: (026) 2323332

WASHIRIKA

ZAECA
EAAACA
IAACA
AAACA
CAACC

WAGENI

31
Visitors Today

Sera ya Faragha
© 2023 TAKUKURU

No Result
View All Result
  • MWANZO
  • KUHUSU SISI
    • SALAMU ZA MKURUGENZI MKUU
    • HISTORIA YA TAASISI
    • MUUNDO WA TAASISI
    • OFISI ZETU
  • UZUIAJI RUSHWA
  • UELIMISHAJI
  • UCHUNGUZI
  • WASHIRIKA
  • MACHAPISHO
  • TAARIFA KWA UMMA
  • BLOG

Sera ya Faragha
© 2023 TAKUKURU