TAKUKURU
No Result
View All Result
  • MWANZO
  • KUHUSU SISI
    • SALAMU ZA MKURUGENZI MKUU
    • HISTORIA YA TAASISI
    • MUUNDO WA TAASISI
    • OFISI ZETU
  • UZUIAJI RUSHWA
  • UELIMISHAJI
  • UCHUNGUZI
  • WASHIRIKA
  • MACHAPISHO
  • E-Huduma
  • BLOG
Taarifa kwa Umma
  • MWANZO
  • KUHUSU SISI
    • SALAMU ZA MKURUGENZI MKUU
    • HISTORIA YA TAASISI
    • MUUNDO WA TAASISI
    • OFISI ZETU
  • UZUIAJI RUSHWA
  • UELIMISHAJI
  • UCHUNGUZI
  • WASHIRIKA
  • MACHAPISHO
  • E-Huduma
  • BLOG
No Result
View All Result
TAKUKURU
No Result
View All Result
Home Taarifa kwa Umma

KUTOKA MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI TANGA.

KUTOKA MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI TANGA.

Juni 26, 2023, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoani Tanga, Mbele ya Mh. Sophia Salim Masati – Hakimu Mkazi, imefunguliwa kesi ya Uhujumu Uchumi Nambari Ecc.09/2023, Jamhuri dhidi ya;
(a) William John Nguruko, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mabokweni;
(b) Sudi Sungura Mshamu, Karani wa Fedha wa Shule ya Msingi Mabokweni;
(c) Mwanabakari Saidi Athumani-Mjumbe wa Kamati ya Shule ya Msingi Mabokweni;
(d) Yusufu Constantine Mushi, Mwalimu Shule ya Msingi Saruji na
(e) Herieth Audax Mwiki ambaye ni Mke wa Sudi Sungura Mshamu.

Washtakiwa hao wamefikishwa Mahakamani kwa makosa 33 ya Rushwa na Uhujumu Uchumi yakiwa ni pamoja na Ubadhilifu na Ufujaji wa Fedha Kiasi Cha Sh.28,382,565/=, kinyume na Kifungu cha 28 (1) na (2) Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura ya 329 Marejeo ya Mwaka 2022, ikisomwa pamoja na aya ya 21 jedwali la kwanza na Kifungu cha 57(1) na 60(2) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi Sura ya 200 Marejeo ya Mwaka 2022, Kula Njama kutenda Makosa ya Rushwa kinyume na Kifungu cha 32 Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura ya 329 Marejeo ya Mwaka 2022, ikisomwa pamoja na aya ya 21 jedwali la Kwanza na Kifungu cha 57(1) na 60(2) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi Sura ya 200 Marejeo ya Mwaka 2022, Makosa ya kughushi Kinyume na Kifungu Cha 333, 335, 337 na 338 na 340 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 Marejeo ya Mwaka 2022 pamoja na Kuisababishia Mamlaka iliyoainishwa Kisheria Hasara ya Sh 28,382,565/= kinyume na aya ya 10(1) jedwali la Kwanza na Kifungu cha 57(1) na 60(2) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi Sura ya 200 Marejeo ya Mwaka 2022.

Kati ya Washtakiwa hao, William John Nguruko na Mwanabakari Saidi Athumani, walikana makosa yote. Yusufu Constantine Mushi alikiri au alikubali kosa la Kujipatia Manufaa ya Sh.16,066,540/= kinyume na Kifungu cha 23 Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura ya 329 Marejeo ya Mwaka 2022, ikisomwa pamoja na aya ya 21 jedwali la Kwanza na Kifungu cha 57(1) na 60(2) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi Sura ya 200 Marejeo ya Mwaka 2022 na pia Mshtakiwa Sudi Sungura Mshamu alikiri au alikubali Makosa yote 32 kama alivyosomewa Hati ya Mashtaka.

Washtakiwa walitenda makosa hayo katika utekelezaji Miradi ya Ujenzi wa Madarasa na Vyoo katika Shule ya Msingi Mabokweni.

Washtakiwa wote wamepelekwa rumande kufuatia wenzao Sudi Sungura Mshamu na Yusufu Constantine Mushi kuomba kusomewa mashitaka upya ili wajibu upya, kwa madai kwamba waliposomewa mwanzo walikubali bila kuelewa.

Mheshimiwa Hakimu aliahirisha kesi hadi Juni 26, 2023 kwa ajili usikilizwaji wa hoja za awali.

ShareTweetSendShare

Taarifa kwa Umma

KUTOKA MAHAKAMANI SAME KILIMANJARO

KUTOKA MAHAKAMANI ROMBO KILIMANJARO

KUTOKA MAHAKAMANI TABORA

KUTOKA MAHAKAMANI TABORA

HAFLA YA KUFUNGA MAFUNZO

CYBER FORENSIC TRAINING

KUTOKA MAHAKAMA YA WILAYA YA IGUNGA- TABORA.

KUTOKA MAHAKAMA YA WILAYA YA IGUNGA- TABORA.

Habari Motomoto

  • National Governance and Corruption Survey (NGACS) 2020

    National Governance and Corruption Survey (NGACS) 2020

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFUNZO YA AWALI YA UCHUNGUZI YAMEHITIMISHWA RASMI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaotafutwa na TAKUKURU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFUNZO YA “INTERMEDIATE INVESTIGATION COURSE” YAFUNGULIWA RASMI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KIKAO CHA USHIRIKIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

WASILIANA NASI

MKURUGENZI MKUU
TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA
NA RUSHWA
S. L. P 1291
41101 Mtaa wa Jamhuri,
DODOMA, Tanzania
Simu: (026) 2323316
Nukushi: (026) 2323332

WASHIRIKA

ZAECA
EAAACA
IAACA
AAACA
CAACC

WAGENI

1515
Visitors Today

© 2022 TAKUKURU

No Result
View All Result
  • MWANZO
  • KUHUSU SISI
    • SALAMU ZA MKURUGENZI MKUU
    • HISTORIA YA TAASISI
    • MUUNDO WA TAASISI
    • OFISI ZETU
  • UZUIAJI RUSHWA
  • UELIMISHAJI
  • UCHUNGUZI
  • WASHIRIKA
  • MACHAPISHO
  • TAARIFA KWA UMMA
  • BLOG

© 2022 TAKUKURU