KUTOKA MAHAKAMANI HAI – KILIMANJARO

Mei 29, 2023 Shauri la Uhujumu Uchumi Na 4.2023 dhidi ya Afisa wa TANESCO Bw. DAVID KISEY lilifunguliwa katika Mahakama ya Wilaya ya Hai.

Mshtakiwa anakabiliwa na makosa 3 ambayo ni ubadhirifu, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu na matumizi mabaya ya mamlaka .

Mshtakiwa akiwa mwajiriwa wa TANESCO kwa vipindi tofauti tofauti mwaka 2022, alijipatia kiasi cha sh. 760,000= kutoka kwa mteja akimdanganya kwamba angempatia huduma ya umeme.

Aidha mshtakiwa amekana makosa yote na yupo nje kwa dhamana.

Shauri litakuja kwa masikilizo ya awali Juni 14.2023.

Taarifa kwa Umma

WAZIRI SIMBACHAWENE ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA JENGO LA TAKUKURU MKOA WA IRINGA .