SONGWE, OKT – DES 2021

TAKUKURU SONGWE YADHIBITI IDARA YA AFYA

 (PORT HEALTH) MPAKA WA TUNDUMA

Ndugu Wanahabari,

Ninawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Nimewaita hapa siku hii ya leo kwa ajili ya kuuhabarisha umma kupitia kwenu Wanahabari, kuhusu Utendaji Kazi wa Ofisi ya TAKUKURU Mkoa wa Songwe kwa kipindi cha Oktoba-Disemba, 2021.

Ndugu Wanahabari,

UZUIAJI RUSHWA

Katika kipindi husika, ofisi ya TAKUKURU Mkoa wa Songwe kupitia Kituo Maalumu cha TAKUKURU Tunduma, imefanya udhibiti wa mianya ya rushwa Idara ya Afya Mpaka wa Tunduma (Port Health).

Kwamba, katika Mpaka wa Tunduma, Idara ya Afya hutoa huduma ya chanjo kwa wasafiri wanaoingia nchini kupitia Mpaka huo wa Tunduma.

Chanjo ambazo hutolewa ni pamoja na Chanjo ya Homa ya Manjano (Yellow Fever); Homa ya Ini aina ya B (Hepatitis B); pia hupima UVIKO 19 kwa wasafiri wasio na cheti cha kipimo cha UVIKO 19; pamoja na upulizaji wa dawa ya kuuwa wadudu kwenye vyombo vya usafiri.

Huduma hizi zote ambazo zinazotolewa na Idara ya Afya Mpaka wa Tunduma zina gharama ambazo zinatakiwa kulipwa na msafiri anayeingia nchini ambaye hana cheti husika kulingana na masharti ya kuingia Nchini. Hivyo ili kuweza kupatiwa chanjo husika, msafiri atatakiwa kulipa kupitia mfumo wa GePG (“Government e-Payment Gateway System”), baada ya kuandaliwa namba ya malipo (“Control number”) ndipo aweze kupatiwa chanjo au huduma husika.

Katika udhibiti huu, ilibainika kuwa Idara ya Afya Mpaka wa Tunduma wakati mwingine hupokea fedha taslimu kutoka kwa wasafiri, badala ya kuwaandalia namba ya malipo ili wasafiri wao wenyewe walipe kwa kutumia mfumo wa GePG.

Wakati udhibiti huu ukifanyika, fedha taslimu kiasi cha Shs. 2,220,000.00 pamoja na Dola za Kimarekani 200 zilikutwa zikiwa zimepokelewa na Watumishi wa Mpaka wa Tunduma – Idara ya Afya toka kwa wasafiri ambao walipatiwa huduma mbalimbali katika Mpaka huo. 

Baada ya udhibiti huu kufanyika na kukamilika, fedha kiasi cha Shs. 2,220,000.00 pamoja na Dola za Kimarekani 200 zililipwa kwa kutumia mfumo wa GePG.

Ndugu Wanahabari,

Pamoja na kufanya udhibiti wa Idara ya Afya Mpaka wa Tunduma, katika kipindi husika Dawati la Uzuiaji Rushwa ambalo hufanya Chambuzi za Mifumo ya Taasisi na Idara mbalimbali za Serikali ikiwa na lengo la kuzuia mianya ya Rushwa inayojitokeza kwenye mifumo ya kiutendaji pamoja kutembelea na kufanya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kwa kushirikiana na wadau pamoja na wananchi ambao ndio wanufaika wa miradi husika, lilifanya kazi zifuatazo:

Tuliweza kufanya jumla ya chambuzi za mifumo mitatu katika ofisi zetu za mkoa wa Songwe. Chambuzi zilizofanyika ni pamoja na:

  1. Uchambuzi wa mfumo katika sekta ya Elimu ambao ulilenga kubaini Viashiria vya Rushwa ya Ngono kwa shule za Msingi na Sekondari.

Uchambuzi huu ulibaini kuwepo kwa mianya mingi ya rushwa katika sekta ya elimu ambayo inachochewa na ukiukwaji wa maadili ya kitaaluma na maeneo yanayochochea rushwa hiyo ni katika upangaji wa vituo vya kazi, uhamisho wa ndani ya halmashauri pamoja na utoaji wa fursa za mafunzo ya muda mfupi na mrefu pamoja na uteuzi kufanya kazi maalum. Ofisi yetu inatarajia kufanya warsha na wadau wanaohusika na uchambuzi huu ili kujadili namna ya kuziba mianya hiyo.

  • Uchambuzi wa mfumo wa mianya ya Rushwa katika mfumo wa Manunuzi ya Umma kupitia GPSA.

Uchambuzi huu umebaini kuwa taasisi nyingi za Serikali hazifanyi manunuzi kupitia Wakala wa Manunuzi ya Umma (GPSA) na kwamba ofisi yetu itafanya warsha na wadau husika ili kujadili namna ya kuziba mianya hiyo.

Vilevile, tuliweza kutembelea na kukagua utekelezaji wa jumla ya miradi ya maendeleo mitatu yenye thamani ya Shs.791,197,546 Miradi hi iimekaguliwa kwa kushirikiana na wadau husika wa miradi pamoja na wananchi ambao ndio wanufaika wa miradi husika. Miradi hiyo ilijumuisha:

  • Mradi wa ujenzi barabara ya vwawa mjini kwa kiwango cha lami KM 1 yenye thamani ya Tsh. 449,285,470
  • Ufuatiliaji wa matumizi ya fedha za uhamasishaji wa zoezi la chanjo katika ofisi ya Katibu Tawala (RAS) Mkoa wa Songwe na Halmashauri ya wilaya ya Mbozi wenye thamani ya Tshs. 121,000,000/=
  • Ukamilishaji wa zahanati ya Mtunduru, kata ya Magamba Wilaya ya Mbozi wenye thamani ya Shs. 50,000,000/=;

Vilevile, tuliweza kutembelea na kukagua utekelezaji wa jumla ya miradi ya maendeleo 16 iliyotokana na fedha za Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO 19 yenye thamani ya Shs. 840,000,000/=.

Miradi hii iimekaguliwa kwa kushirikiana na wadau husika wa miradi pamoja na wananchi ambao ndio wanufaika wa miradi husika. Miradi hiyo ilijumuisha:

  • Ujenzi wa vyumba 04 vya madarasa shule ya Sekondari Muungano; Majengo; DANIDA na J.K. Nyerere wenye thamani ya Shs. 80,000,000.00 kila mmoja
  • Ujenzi wa bweni shule ya msingi Kitete H/Mji Tunduma wenye  Thamani ya Tsh 80,000,000.00   
  • Ujenzi wa vyumba 02 vya madarasa na Ofisi 01 katika shule za Sekondari Bubigu; Itumba;  Luswiswi; Mlale; Steven Kibona; Wilaya ya Ileje wenye thamani ya Shs. 40,000,000.00 kila mmoja
  • Ujenzi wa vyumba 03 vya madarasa na Ofisi 01 katika shule za Sekondari Ikinga; Ileje; Kafule na  Nakalulu Wilaya ya Ileje wenye thamani ya Shs. 60,000,000.00 kila mmoja
  • Ujenzi wa vyumba 03 vya madarasa na Ofisi 01 katika shule ya Sekondari Shinji Wilaya ya Ileje wenye thamani ya Shs. 80,000,000.00
  • Ujenzi wa vyumba 02 vya madarasa na Ofisi 01 katika vituo shikizi vya Shule za Msingi za Lusungo; Mangwina; Ibandi na Ipesi Wilaya ya Ileje wenye thamani ya Shs. 40,000,000.00 ki