MTWARA, OKT – DES 2021

KAMPENI YA UWAJIBIKAJI YALETA TIJA MIRADI YA MAENDELEO MKOA WA MTWARA

UTANGULIZI:

Ndugu Waandishi wa Habari,

Nimewaita hapa kwa lengo la kuujulisha umma juu ya utendaji kazi wa TAKUKURU Mkoa wa Mtwara kwa kipindi cha Oktoba, 2021 hadi Desemba, 2021.Utaratibu huu ni wa kawaida ambao TAKUKURU imejiwekea ili kuhakikisha kuwa umma wa Watanzania pamoja na wakazi wa mkoa wa Mtwara wanafahamu jitihada zinazofanywa na Serikali katika kuzuia na kupambana na rushwa.

Ndugu Waandishi wa Habari,

UZUIAJI RUSHWA – Kampeni Maalum:

TAKUKURU Mkoa wa Mtwara, ilianzisha kampeni tunayoiita “Wajibika, chukua hatua stahiki kuzuia rushwa”. Lengo kuu la kampeni hii ni kubadili tabia ya walengwa kutoka kuwa walalamikaji hadi kufikia hatua ya kuchukua hatua stahiki kwa yale yaliyo katika mamlaka au uwezo wao. Katika kampeni hii tulifanikiwa kuwafikia wadau mbalimbali ikiwemo waheshimiwa madiwani katika Halmashauri zetu, kamati zinazo husika na miradi ya maendeleo na wananchi kiujumla, kupitia semina,vipindi vya redio na uelimishaji  maeneo ya miradi.

Katika utekelezaji wa ujenzi wa madarasa haya tulishuhudia ushirikiano wa hali ya juu sana kwanza kwa viongozi ngazi ya Mkoa, Wilaya na   Halmashauri.  Kamati zilizohusika na miradi pamoja na wananchi na viongozi wa maeneo husika walionesha ushirikiano mkubwa. Kwa ushirikiano huu changamoto nyingi zilizojitokeza zilitatuliwa na ushauri kutoka kwa wataalam na wadau ulitolewa mapema kwa wahusika.

  • Kulikuwa na uwazi mkubwa kwa maana wananchi walijua kiasi cha fedha kilichotengwa kwaajili ya shughuli husika.
  • Fedha zilifika kwa walengwa kwa wakati na kwa kiwango chote.
  • Maamuzi ya kununua baadhi ya vifaa kama saruji, mabati, vigai (tiles) na mbao kwa wingi na kwa pamoja (bulk purchase) kutoka viwandani na kwenye chanzo kimoja, ulileta tija ya ubora wa vifaa, kupunguza gharama na upatikanaji wa vifaa kwa wakati nakufanya kazi zinazoweza kufanyika kwa wakati mmoja kufanyika na hivi kumaliza miradi kwa wakati.
  • Kasoro mbalimbali zilizokuwa zinagundulika zilishughulikiwa kwa wakati. 

Miradi yote ikifanyika kwa ushirikiano na uwazi wa kiwango hiki na kama kila mmoja wetu atachukua hatua stahiki iliyo ndani ya uwezo wake katika kushiriki ujenzi, kulinda miradi,  kufuatilia matumizi ya fedha katika miradi hii na kuhakikisha kuna uwazi na uwajibikaji, Mkoa wa Mtwara utapiga hatua kubwa zaidi ya maendeleo.  

Ndugu Waandishi wa Habari,

UENDESHAJI WA MASHTAKA:

Katika kipindi cha Oktoba 2021 hadi Desemba 2021, kesi sita (6) ziliendelea mahakamani na Kesi tatu (3) zilitolewa maamuzi ambapo Jamhuri ilishinda katika kesi mbili (2).

Ndugu Waandishi wa Habari, 

UCHUNGUZI:

Katika kipindi cha  Oktoba, 2021 hadi Desemba, 2021, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mtwara iliendelea na utekelezaji wa majukumu yake ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa kama yalivyotamkwa katika kifungu cha 7 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa sura ya 329 iliyorejewa mwaka 2019.

Katika kipindi tajwa jumla ya malalamiko (77) yalipokelewa TAKUKURU (M) Mtwara. Kati ya malalamiko hayo 77, malalamiko 57 yalihusu rushwa na malalamiko 20 hayakuhusu rushwa. Malalamiko 57 yaliyohusu rushwa yanafanyiwa uchunguzi ili kuthibitisha makosa ya rushwa na uchunguzi wake bado unaendelea. Kwa Malalamiko 20 ambayo hayakuhusu rushwa, wahusika walishauriwa namna bora ya kupata haki zao. Hakukuwa na taarifa ambayo ilihamishiwa idara nyingine.

Mchanganuo wa Sekta au taasisi zinazolalamikiwa ni kama ifuatavyo:-

Halmashauri malalamiko (49) katika idara zake kwa mchanganuo ufuatao:- afya(21), utawala (8), elimu (6), ardhi (6), Ujenzi (3),  biashara(2), Maji (2) na manunuzi (1).

Malalamiko mengine ni vyama vya Ushirika malalamiko (9), Polisi (5), mahakama (3), Magereza (1), Benki (1), viwanda (1) na binafsi (8).

Ndugu Waandishi wa Habari.

UZUIAJI RUSHWA:

katika kipindi tajwa, ili kuzuia Rushwa, tumefuatilia matumizi ya fedha za umma katika utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa hapa mkoani Mtwara.

Lengo likiwa ni kuhakikisha kwamba miradi hiyo inatekelezwa kwa kiwango kinachotakiwa na thamani ya fedha inapatikana.

Jumla ya miradi ya maendeleo 114  yenye thamani ya jumla ya shilingi 6,937,500,000/= ilifuatiliwa kama ilivyoainishwa kwenye jedwali hapa chini:-

Miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa yatokanayo na Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO 19 :-

NAMRADITHAMANI  (Tsh)
1.Ujenzi wa vyumba vya madarasa 109 katika shule 44 tofauti wilaya ya Mtwara.2,180,000,000/=
2.Ujenzi wa vyumba vya madarasa  82 katika shule 21 tofauti wilaya ya Tandahimba1,640,000,000/=
3.Ujenzi wa vyumba vya madarasa 80 katika shule 21 tofauti wilaya ya Masasi.1,600,000,000/=
4.Ujenzi wa madarasa 24 katika shule 5 tofauti wilaya ya Nanyumbu480,000,000/=
JUMLA5,900,000,000/=

Pia , umefanyika ufuatiliaji wa miradi mingine kama ilivyoainishwa kwenye jedwali hapo chini:-

NAMRADITHAMANI
1.Ujenzi wa OPD na Maabara kituo cha Afya ufukoni wilaya ya Mtwara.250,000,000/=
2.