TAKUKURU
  • MWANZO
  • KUHUSU SISI
    • HISTORIA YA TAASISI
    • SALAMU ZA MKURUGENZI MKUU
  • UZUIAJI RUSHWA
  • UELIMISHAJI
  • UCHUNGUZI
  • WASHIRIKA
  • MACHAPISHO
  • OFISI ZETU
Taarifa kwa Umma
No Result
View All Result
  • MWANZO
  • KUHUSU SISI
    • HISTORIA YA TAASISI
    • SALAMU ZA MKURUGENZI MKUU
  • UZUIAJI RUSHWA
  • UELIMISHAJI
  • UCHUNGUZI
  • WASHIRIKA
  • MACHAPISHO
  • OFISI ZETU
No Result
View All Result
TAKUKURU
No Result
View All Result
Home Repository

MBEYA, OKT – DES 2021

TAKUKURU MBEYA YASHIRIKIANA NA SKAUTI KATIKA UZUIAJI RUSHWA

Ndugu Wanahabari.

Leo tumekutana tena katika ofisi yetu ya TAKUKURU mkoa wa Mbeya ili kupitia ninyi tuweze kuuhabarisha umma kuhusu utendaji kazi wa ofisi yetu kwa kipindi cha miezi mitatu kuanzia mwezi wa Oktoba 2021 hadi Disemba 2021.

Kwa mujibu kifungu cha 7 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11 ya mwaka 2007, TAKUKURU inayo majukumu makuu matatu ambayo ni; Kuelimisha Jamii kuhusu rushwa na madhara yake; Kufanya chambuzi za mifumo kwenye taasisi za umma na sekta binafsi pamoja na kufanya uchunguzi na kwa kibali cha Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), kufikisha watuhumiwa mahakamani.

Ndugu Wanahabari

Ushirikiano na SKAUTI

Katika kipindi hiki, TAKUKURU Mkoa wa Mbeya kupitia ushirikiano wa TAKUKURU NA CHAMA CHA SKAUTI TANZANIA (TAKUSKA), ilifanya kazi kubwa mbili ambazo ni zifuatazo:

  • Kuandaa Mpango wa Kazi wa namna ya  kutekeleza Mwongozo wa Mafunzo kwa Wawezeshaji wa Kufundisha Vijana wa Skauti kuhusu Kuzuia na Kupambana na Rushwa na
  • Kuendesha Mashindano ya Ligi ya Mpira wa Miguu, Mpira wa Pete na Mchezo wa Kuvuta Kamba – TAKUSKA SUPPER CUP. 

Ndugu Wanahabari

Tarehe 15/11/2021, Mpango wa Kazi wa kutekeleza Mwongozo wa Mafunzo kwa Wawezeshaji wa Kufundisha Vijana wa Skauti Kuhusu Kuzuia na Kupambana na Rushwa ulizinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera. Uzinduzi wa Mpango wa Kazi huo ulienda sambamba na kupewa mafunzo kwa Viongozi wa Skauti kutoka wilaya zote za Mkoa wa Mbeya.

  • Mafunzo yalitolewa na Maafisa Uchunguzi kutoka TAKUKURU Mkoa wa Mbeya ambapo wakuu wa madawati ya Uzuiaji Rushwa, Elimu kwa Umma, Uchunguzi na Intelijensia yaliwasilisha mafunzo hayo.
  • Mada zilizowasilishwa ni:
  • Madhara ya Rushwa katika jamii pamoja na
  • Namna ya kutoa taarifa TAKUKURU kwa kazi za TAKUSKA.

Jumla ya washiriki katika mafunzo haya walikuwa ni 95 ambapo wavulana ni 65 na wanawake 30.

  • Mashindano ya TAKUSKA SUPER CUP yalizinduliwa rasmi tarehe 22/12/2021 katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Iyunga, Mgeni Rasmi akiwa ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ambaye aliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya Mhe. Dkt. Mohamed Rashid Chuachua.
  • Mashindano haya yameshirikisha jumla ya Tarafa tano za Wilaya ya Mbeya ambazo ni Tarafa ya Iyunga, Sisimba, Usongwe, Tembela na Isangati.
  • Michezo iliyoshindanishwa ni Mpira wa Miguu, Mpira wa Pete, Kuvuta Kamba, Mashairi, Nyimbo pamoja na Ngonjera.
  • Lengo la mashindano ya TAKUSKA SUPER CUP lilikuwa ni kuhamasisha vijana kujiunga na SKAUTI pamoja na Klabu za Wapinga Rushwa ili wapewe mafunzo na elimu ya mapambano dhidi ya rushwa. Tunafanya hivyo tukiamini kuwa vijana hao wakielimika wataweza kuibua taarifa za vitendo vya rushwa katika jamii ikiwemo taarifa zitakazohusu utekelezaji wa Miradi itakayojengwa chini ya kiwango.
  • Pili ni kutoa elimu ya mapambano dhidi ya rushwa kwa washiriki wa michezo na jamii inayofika katika sehemu/viwanja vya michezo kushuhudia michezo hiyo.
  • Kupitia mashindano TAKUSKA Super Cup imefanikiwa kutoa elimu ya mapambano dhidi ya rushwa katika mikutano kumi (10) na vipindi vya redio vitano kwenye tarafa tano ambapo jumla ya vijana 1055 wamejiunga na skauti na jumla ya wananchi 1624 walipata elimu ya mapambano dhidi ya rushwa.

Ndugu Wanahabari

UCHUNGUZI

Katika kipindi cha Oktoba hadi Disemba 2021, TAKUKURU Mkoa wa Mbeya imeweza kutekeleza majukumu yake ya uchunguzi na kufanikiwa kupokea jumla ya taarifa mpya 109 za tuhuma za rushwa na makosa mengine. Taarifa 69 zilihusu rushwa na taarifa 40 hazikuhusu rushwa.

Taarifa 63 zilizohusu rushwa zimefunguliwa majalada ya uchunguzi.

  • Majalada sita (6) yamekamilika
  • Majalada matano (5) yamepelekea kufungua majalada ya kesi mahakamani,
  • Majalada hamsini na mbili (52) uchunguzi wake unaendelea

Katika taarifa arobaini (40) ambazo hazikuhusu rushwa, taarifa 22 watoa taarifa wake walielimishwa na kushauriwa mamlaka sahihi ya kuwasilisha taarifa zao na taarifa kumi na nane (18) zilihamishiwa idara nyingine.

Mchanganuo wa kisekta na idadi kwa malalamiko yote 109 iko kama ifuatavyo kwenye jedwali hapo chini

NaIdaraIdadi
1Halmashauri20
2Mahakama12
3Polisi5
4Afya8
5Sekta binafsi (wafanyabiashara)20
6Ardhi12
7Mashirika ya Umma12
9Vyama vya Ushirika4
10Ujenzi2
15Maliasili5
16Elimu7
17Fedha2
 Jumla109

Ndugu Wanahabari

MASHTAKA

Kwa upande wa Mashtaka, katika kipindi hiki, tumeweza kufungua kesi mpya kumi na mbili (12) Mahakamani kwa makosa mbalimbali na kufanya tuwe na kesi 57 zilizoendeshwa mahakamani katika kipindi tajwa. Hata hivyo Katika kipindi hicho kesi zilizoamuliwa mahakamani ni 18 ambapo kati ya hizo TAKUKURU imeshinda kesi 12 na kushindwa kesi 6.

Ndugu Wanahabari

UZUIAJI RUSHWA

Katika kipindi cha Oktoba – Desemba 2021, kwa upande wa Uzuiaji Rushwa, TAKUKURU Mkoa wa Mbeya imefanikiwa kufanya chambuzi za mfumo sita (6) ambazo zilifanyika katika Sekta ya Elimu katika Shule za Msingi na Sekondari, Usimamizi wa Mitihani katika Vyuo vya Kati na Utawala.

Mapungufu yaliyobainika ni kutokuzingatiwa kwa Mwongozo wa Usimamizi wa Mitihani. Ili kuidhibiti hali hiyo, Kikao kati ya TAKUKURU Mkoa wa Mbeya na wadau husika kilifanyika na kuweka mikakati ya namna ya kurekebisha mapungufu haya.

Ndugu Wanahabari

Vilevile, katika kipindi tajwa TAKUKURU Mkoa wa Mbeya ilifuatilia utekelezaji wa miradi 44 ya maendeleo yenye thamani ya jumla ya shilingi Bilioni saba, milioni miatatu na themanini na sita, laki tano ishirini na saba, mia nane themanini na mbili nukta sita tisa (7,386,527,882.69) katika Sekta za Afya, Elimu, Maji na Barabara ikiwemo miradi inayotekelezwa kupitia fedha za Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO – 19 (Maarufu Miradi ya UVIKO). Lengo la ufuatiliaji huu lilikuwa ni kuhakikisha kuwa miradi inayotekelezwa, inatekelezwa kwa wakati ikiwa na ubora unaolingana na thamani ya fedha iliyotolewa.

Miradi ya Maendeleo endelevu inategemea rasilimali fedha na  bidhaa, nguvu kazi, mawazo na  ushiriki  wa dhati  na adilifu wa kila mwananchi, asasi za kiraia, sekta binafsi, asasi zisizo za Serikali, nchi wahisani na  Serikali. Kila mmoja kati ya wadau hawa ana wajibu wa kuzuia na kupambana na rushwa katika utekelezaji wa miradi hiyo ili kuhakikisha malengo ya miradi ya maendeleo yanafikiwa. Ikumbukwe kuwa maendeleo ya nchi huletwa na wananchi   wenyewe, ambao ni wewe na mimi.  

Mapungufu yaliyobainika katika ufuatiliaji wa miradi hiyo yanahusisha maeneo yafuatayo:

  • Ujazaji wa vitabu vya kuingiza na kutolea vifaa vya ujenzi;
  • Uchelewaji wa kuanza kwa ujenzi jambo ambalo hupelekea ujenzi kuchelewa kumalizwa kwa wakati na kusababisha huduma kuchelewa kutolewa kwa wananchi.

TAKUKURU mkoa wa Mbeya ilitoa ushauri ikiwa ni njia moja wapo ya kufanya uzuiaji wa vitendo vya rushwa kutokea hivyo mapungufu hayo yalifanyiwa kazi. Vilevile, elimu imetolewa kwa wadau husika kwa lengo la kuondoa mianya ya rushwa iliyopo na kuimarisha usimamizi wa miradi hiyo hasa kwa kusisitiza uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na Taratibu za Manunuzi ya Umma.

Katika hatua nyingine, katika kipindi tajwa TAKUKURU Mkoa wa Mbeya ilianzisha operation maalumu ambayo imepewa jina la KATA KWA KATA katika Kata za Itezi, Nonde, Ilomba, Nsalaga na Sisimba.

Kata hizo zote ni za Wilaya ya Mbeya.

Katika kata hizo tumefanya yafuatayo:

  • Utambuzi wa Miradi ya Serikali Kuu,
  • Utambuzi wa Miradi inayoendeshwa na Halmashauri kupitia fedha za ndani,
  • Utambuzi wa Miradi inayoendeshwa na wafadhili,
  • Tumepokea taarifa za malalamiko ya wananchi dhidi ya Rushwa na
  • Tumebainisha vyanzo vya mapato ya fedha katika kata hizo.

Baada ya kufanya utambuzi wa miradi hiyo na kuchambua nyaraka mbalimbali, pamoja na mambo mengine, TAKUKURU Mkoa wa Mbeya ilibaini kuwa fedha za utekelezaji wa Miradi hazina usimamizi mzuri na hivyo kufikia hatua ya kutotumika kama ambavyo ilikuwa imekusudiwa.

Ili kuziba mwanya huo ambao ungeweza kusababisha uwepo wa rushwa, TAKUKURU Mkoa wa Mbeya imewaelimisha wahusika wakuu katika usimamizi wa fedha za miradi na pia taarifa ya changamoto hii inaandaliwa ili kuona iwapo kuna haja ya kuanzisha uchunguzi.

Ndugu Wanahabari

ELIMU KWA UMMA

TAKUKURU Mkoa wa Mbeya katika kipindi cha miezi mitatu imeendelea na jukumu la kuelimisha umma kwa kuyafikia makundi mbalimbali ya jamii, lengo likiwa ni kuendelea kuwajengea uelewa wa madhara ya rushwa, ili waweze kushiriki katika mapambano dhidi ya rushwa.

Kupitia uelimishaji huo tumeweza kuwafikia wananchi 2,913 ambao walipata elimu kupitia Semina 11 zilizoandaliwa, Mkutano wa hadhara 01, Maonesho 6 na Klabu za wapinga rushwa 07 za shule za msingi na sekondari – zilizoimarishwa.

Ndugu Wanahabari

TAKUKURU INAYOTEMBEA

TAKUKURU Mkoa wa Mbeya iliendelea na zoezi la kutembelea wananchi katika maeneo yao kwa lengo la kusikiliza kero za rushwa. Katika kipindi cha miezi mitatu tumefanikiwa kupokea kero mbalimbali za rushwa na makosa mengine. Kwa zile taarifa ambazo hazihusiani na rushwa tumekuwa tukiziwasilisha kwenye Mamlaka husika ili ziweze kufanyiwa kazi na wananchi kupewa mrejesho. Kwa kipindi tajwa tumefika katika Kata za Itewe, Kambikatoto pamoja na Lupa.

Ndugu Wanahabari

MATARAJIO YETU KWA KIPINDI CHA MIEZI MITATU IJAYO.

Katika kipindi cha miezi mitatu ijayo kuanzia Januari hadi Machi 2022 tumejipanga kufanya mambo yafuatayo: –

  1. Kuendelea kuelimisha wananchi kuhusu rushwa na madhara yake katika usimamizi wa miradi ya maendeleo katika Kata, Mitaa na Vijiji, lengo likiwa ni kuwawezesha wananchi kupata uelewa na kuweza kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa karibu na kutoa taarifa TAKUKURU pale wanapoona ubadhirifu.
  2. Tutaendelea kutekeleza Mpango Kazi wa TAKUSKA katika mkoa wetu ili tuwafikie vijana wengi zaidi.
  3. Tutaendelea kufanya kazi za uzuiaji rushwa kwa lengo la kubaini mianya ya rushwa katika maeneo mbalimbali zikiwemo Taasisi za Umma na Binafsi na kushauri namna bora ya kuiziba mianya hiyo.

Pia natoa rai kwa Wakurugenzi wa Halmashauri zote za mkoa wa Mbeya, kutoa ushirikiano wa wakati wa  kutekeleza miradi ya Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO -19 katika Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa pindi utakapo hitajika.

  • Tutaendelea kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua wale wote watakao kutwa na tuhuma za vitendo vya rushwa ikiwa ni pamoja na kuwafikisha Mahakamani.
  • Pamoja na Serikali kuweka sheria nyingi na kali bado taaarifa nyingi ambazo zimekuwa zikipokelewa kwenye ofisi za TAKUKURU (M) Mbeya zimekuwa zikiwagusa sana Watendaji wa Kata, Madiwani, Wenyeviti wa Vijiji  na Mitaa na viongozi wengine wa ngazi ya Kata.
  • Baadhi ya viongozi wamekuwa wakitumia udhaifu wa wananchi kutojua sheria na hivyo kuwakandamiza au kuwanyima haki zao za msingi. Hivyo TAKUKURU Mkoa wa Mbeya itaendesha operation ya KATA KWA KATA ili kubaini yafuatayo:-
  • Kuchunguza ufanisi wa matumizi ya sheria na miongozo mbalimbali iliyotolewa kuhusu uongozi kwenye ngazi ya Kata.
  • Kubaini mianya ya rushwa katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku ya viongozi wa Kata za mkoa wa Mbeya.
  • Kubaini changamoto za upatikanaji wa huduma kwa wananchi wa mkoa wa Mbeya kwenye ngazi ya kata.
  • Kubaini thamani ya fedha katika miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwenye kata ikilinganishwa na hali halisi ya mradi unavyoonekana.
  • Kubaini vitendo na ubadhirifu wa fedha ambavyo vinaangukia kwenye Sheria ya Kuzuia na Kupambana na rushwa Na. 11/2007
  • Kubaini aina ya elimu ya rushwa inayohitajika kuwapatia wananchi wa kata husika.

Ndugu Wanahabari

Baada ya kusema hayo, nipende kuwapongeza wananchi wote wa Mkoa wa Mbeya kwa jinsi wanavyoendelea kushirikiana na TAKUKURU katika kufichua vitendo vya rushwa. Ninawasihi kuendelea kushirikiana na TAKUKURU kwa kutoa taarifa za vitendo vya rushwa, nasi tunaahidi kuzifanyia kazi taarifa tutakazo zipokea kwa wakati.

Imetolewa na:

DENIS MANUMBU

MKUU WA TAKUKURU MKOA WA MBEYA

Nambari ya simu: SIMU BURE 113

MKUU WA TAKUKURU (M) 0738 150137

NAIBU MKUU WA TAKUKURU (M) 0738 150 138

ShareTweetSendShare

Taarifa kwa Umma

HAFLA YA KUFUNGA MAFUNZO

CYBER FORENSIC TRAINING

MAZUNGUMZO

MAZUNGUMZO

MAELEKEZO

ZIARA

DG PCCB

MKURUGENZI MKUU WA TAKUKURU CP. SALUM RASHID HAMDUNI

Habari Motomoto

  • UZINDUZI WA MWONGOZO WA KUFUNDISHA SKAUTI

    UZINDUZI WA MWONGOZO WA KUFUNDISHA SKAUTI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TAARIFA YA UTENDAJI KAZI 2020/2021

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MKURUGENZI MKUU WA TAKUKURU CP. SALUM RASHID HAMDUNI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAELEKEZO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Takwimu za uchunguzi kuanzia mwaka 2005 hadi 2014

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

WASILIANA NASI

MKURUGENZI MKUU
TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA
NA RUSHWA
S. L. P 1291
41101 Mtaa wa Jamhuri,
DODOMA, Tanzania
Simu: (026) 2323316
Nukushi: (026) 2323332

WASHIRIKA

ZAECA
EAAACA
IAACA
AAACA
CAACC

© 2022 TAKUKURU

No Result
View All Result
  • MWANZO
  • KUHUSU SISI
    • HISTORIA YA TAASISI
    • SALAMU ZA MKURUGENZI MKUU
  • UZUIAJI RUSHWA
  • UELIMISHAJI
  • UCHUNGUZI
  • WASHIRIKA
  • MACHAPISHO
  • OFISI ZETU
  • TAARIFA KWA UMMA

© 2022 TAKUKURU