Kampeni imejengengeka kwenye dhana ya ushirikiano wa makundi muhimu katika kupambana na ajali za barabarani Makundi hayo ni TAKUKURU, Jeshi la Polisi na Wadau; Neno “Wadau” linajumuisha makundi mbalimbali; Hatuhitaji kumnyooshea kidole mtu au taasisi yoyote bali kukaa pamoja kutatua kero za ajali za barabarani. Tatizo la ajali za barabarani linasababishwa na mambo mengi ikiwemo RUSHWA, SHERIA MBOVU, UBOVU WA MIUNDOMBINU n.k. Tunahitaji kuweka mikakati ya pamoja na endelevu inayotibu tatizo.